MAMLAKA ya Maji safi na Usafi Mazingira Kahama Shinyanga (KASHWASA) wameadhimisha siku ya Wafanyakazi (Meimosi)
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mboni Mhita ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye maadhimisho hayo amesema hajapata malalamiko yoyote
kutoka kwa wafanyakazi huku akiwaomba waendelee kufanya kazi vizuri
zaidi na mazingira yao yakiendelea kuboreshwa.
Mhita
amesema yapo mafanikio mengi yaliyopatikana kwa wafanyakazi ambapo wapo
waliopandishwa madaraja na mazingira ya kazi kuboreshwa pia changamoto
walizozitoa zote ataziwasilisha mahali husika na zilizo ndani ya uwezo
wa mkoa zitafanyiwa kazi.
"Salamu
mlizozitoa kwa Rais nitazifikisha na changamoto kama waajiri kutumia
vibaya mikataba ya wafanyakazi wao na wengine kuzuia kujiunga na vyama
vya wafanyakazi na mfuko wa hifadhi ya jamii (NSSF) kutopeleka
michango na kuchelewesha wastaafu " amesema Mhita.
Mhita
amewatoa hofu watumishi walioko ndani ya mkoa kwani maslahi yao
yanaendelea kuboreshwa ametoa rai waendelee kuwa na weledi kutambua
haki na wajibu inayoendana na waajiri.
Mratibu
wa Shirikisho la vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA) kwa mkoa wa
Shinyanga Ramadhani Pangala amesema wafanyakazi wa sekta binafsi na
serikali waboreshewe maslahi yao kwani wanaipongeza serikali
kuzingatia utoaji wa ajira mpya kwa vijana.
Maadhimisho
hayo yalikuwa na kauli mbiu isemayo kazi zenye staha ni nguzo imara
kwa Maendeleo endelevu katika utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050.



.jpg)


0 Comments