

Na Kareny Masasy, Kahama
MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mboni Mhita amesema hajapata malalamiko yoyote
kutoka kwa wafanyakazi huku akiwaomba waendelee kufanya kazi vizuri
zaidi na mazingira yao yakiendelea kuboreshwa.
Mhita
amesema hayo leo kwenye maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani (Mei
Mosi) yaliyofanyika Manispaa ya Kahama nakuratibiwa mwaka huu na chama
cha walimu Tanzania (CWT).
Mhita
amesema yapo mafanikio mengi yaliyopatikana kwa wafanyakazi ambapo wapo
waliopandishwa madaraja na mazingira ya kazi kuboreshwa pia changamoto
walizozitoa zote ataziwasilisha mahali husika na zilizo ndani ya uwezo
wa mkoa zitafanyiwa kazi.
"Salamu
mlizozitoa kwa Rais nitazifikisha na changamoto kama waajiri kutumia
vibaya mikataba ya wafanyakazi wao na wengine kuzuia kujiunga na vyama
vya wafanyakazi na mfuko wa hifadhi ya jamii (NSSF) kutopeleka
michango na kuchelewesha wastaafu " amesema Mhita.
Mhita
amewatoa hofu watumishi walioko ndani ya mkoa kwani maslahi yao
yanaendelea kuboreshwa ametoa rai waendelee kuwa na weledi kutambua
haki na wajibu inayoendana na waajiri.
Mratibu
wa Shirikisho la vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA) kwa mkoa wa
Shinyanga Ramadhani Pangala amesema wafanyakazi wa sekta binafsi na
serikali waboreshewe maslahi yao kwani ikiwa wanaipingeza serikali
kuzingatia utoaji wa ajira mpya kwa vijana.
Bado
kuna changamoto nyingi pia kuna Tume ya usuluhishi na utumishi
ambayo imekuwa haifanyi kazi ipasavyo kwa kiwango kinachostahili
katika kutatua migogoro kwa watumishi na eneo la bima ya afya kwa
wafanyakazi kupata matibabu kumekuwa na usumbufu.
pangala amesema wafanyakazi wanapotaka kwenda kwenye masomo gharama ni kubwa nakuomba serikali kuondoa kero hiyo.
Maadhimisho hayo yalikuwa na kauli mbiu isemayo kazi zenye staha ni nguzo imara kwa Maendeleo endelevu katika utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050.







0 Comments