Na Kareny Masasy,
Kahama
Wawekezaji nchini wameitwa kuwekeza kwenye kongani ya viwanda iliyopo eneo la Buzwagi Economic Zone Manispaa ya Kahama Mkoani Shinyanga.
Takribani wawekezaji 35 wamejitokeza kuchukua maeneo mbalimbali wakiwemo kampuni ya Kabanga Nickel inayojishugulisha na utengenezaji wa vipuri vya kuchenjua dhahabu na umoja wa Suplier nchini waliochukua eneo lenye ukubwa wa ekari 127.
Kamati ya kudumu ya bunge Utawala,Katiba na Sheria ikiongozwa na mwenyekiti wake Dk Damas Ndumbaro amesema watatumia nafasi waliyonayo kuitangaza kongani zote nchini ikiwemo hii ya Buzwagi Kahama.
"Eneo la kongani Buzwagi tumejionea liko vizuri halina shida yoyote na miundombinu yote imekamilika ikiwemo barabara,maji na umeme nasi tumelizika"
kuwekeza h
kuw

0 Comments