SHULE YA MSINGI IWELYANGULA YAPATA MSAADA WA VYAKULA


 Na  Kareny  Masasy, Shinyanga

WADAU wa Kupinga vitendo vya ukatili manispaa ya Shinyanga  wametoa  msaada wa vyakula mbalimbali ikiwemo kilo 900 za mahidi na sukari kilo 145 katika shule ya msingi  Iwelyangula huku wakiwashauri wazazi kuendelea kutoa mchango wa chakula shuleni.


 Mkurugenzi wa shirika la Rafiki SDO Gerald Ng'ong'a  kwa niaba ya wadau wa kupinga vitendo vya ukatili waliochangia vyakula  hivyo alisema upatikanaji wa chakula kwenye shule hiyo  uwe endelevu huku akiahidi  kutoa kilo 100 za mahindi kila baada  ya miezi mitatu.

 Ngo'ng'a  alisema   wazazi wanatakiwa kuunga mkono  juhudi  hizi kwa kuchangia chakula na mikakati iwepo ya kila robo na utaratibu wa utumikaji wa vyakula shuleni hapo walimu washirikishe wanafunzi waone vimetumikaje.

"Leo  linafanyika zoezi la uzinduzi rasmi wa chakula shule ya  msingi Liwelyangula  wazazi nasi tuchangie libaki jukumu la walimu kufundisha na watoto wetu wafaulu mitihani yao"amesema ng'ong'a.

Mwakilishi kutoka shirika la Invest in Children Society  (ICS) linalojihusisha na masuala ya malezi na makuzi ya mtoto Lucy Maganga akieleza suala la mawasiliano alisema  wazazi wengi wanakosa kuwa na mawasiliano mazuri na watoto hilo ndio gepu kubwa ambalo pia kushindwa kujua mahitaji muhimu ya shule 

Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Iwelyangula Lea Mzava alisema  shule hiyo ina wanafunzi 452  na leo amefurahi maadhimisho ya siku ya wanawake na uzinduzi rasmi wa chakula shuleni  hapa lengo lilikuwa kuhamasisha wazazi kuchangia chakula kwani robo ya wanafunzi ndiyo wamekuwa wakilipiwa chakula.

Mwenyekiti kamati ya shule  Machibya James alisema  kwenye vikao wamekuwa wakisisitiza wazazi kuchangia na sasa wanakuka na mpango mpya mzazi asiyechangia chakula atachukuliwa hatua.

Ofisa maendeleo ya jamii  Manispaa ya Shinyanga  Nyanjura Kiyenze alisema wazazi upo umuhimu wa utoaji chakula shuleni wasipo kula shuleni ni chanzo cha kufanya vibaya darasani igeni mfano wa shule ya msingi Lubaga wazazi wanatoa chakula na wanafunzi wanafanya vizuri.

Mwakilishi kutoka idara ya  Elimu Msingi Manispaa ya Shinyanga Francisca Msindu alisema Serikali imeendelea kuboresha miundombinu ya shule na kuhakikisha wanafunzi wa wanasoma katika mazingira mazuri nakuwataka wazazi wahakikishe chakula shuleni kinapatikana ili kuwaondolea sdha wanafunzi kushinda njaa.


Post a Comment

0 Comments