SERIKALI KUFUATILIA NYUMBA KWA NYUMBA KUFIKIWA NISHATI YA UMEME

 

Na Kareny Masasy,

Kahama

KAMATI ya kudumu ya nishati na Madini imeeleza utekelezaji wa nishati ya umeme kwenye vitongoji vilivyokusudiwa una lizisha huku  zamu ya kuanza kupata nishati ya umeme  nyumba kwa nyumba utaangaliwa zaidi  ili kufikia adhima ya  mwaka 2034 maeneo yote yawe na  nishati hiyo.

Mwenyekiti wa kamati hiyo Subira Mgulu ambaye ni mbunge wa jimbo la Bagamoyo amesema  hayo  juzi kabla ya uzindizi wa uwashaji wa nishati ya umeme kwenye Zahanati iliyopo kitongoji cha Mwaguhuma kata ya Mwakata Halmashauri ya  Msalala na Mashine ya kusaga iliyopo Kagongwa.Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga.

Mgulu amesema serikali imeendelea kusisitiza taasisi kama shule na Vituo vya kutolea huduma za afya viwe na nishati ya umeme kwani wananchi walikuwa wakiteseka sana na kutoa vilio vyao wanapotaka huduma ya kujifungua nyakati za usiku. 

"Hili  suala la ukosefu wa nishati ya umeme kwenye taasisi tumeanza kulifanyia kazi  kwani vijiji vyote hapa kahama tumeelezwa vina nishati ya umeme kazi iliyobaki ni kuwasambazia wananchi kwenye maeneo yao" amesema Mgula.

Mgula amesema  katika bajeti iliyopitishwa mwaka 2025/2026 ilikuwa imelenga katika  kila jimbo vitongoji 15 vipate nishati ya umeme na leo hii  kamati imekuja kukagua nakuona utekelezaji wake ulivyofanikiwa katika vitongoji vilivyoainishwa..

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala Wa Nishati ya Umeme Vijijini (Rea) Jones Olutu  amesema  eneo la wilaya ya Kahama ni miongoni mwa maeneo ya kimkakati  na vijiji vyote  509 vya wilaya ya Kahama vinaumeme ambapo wameendelea kuhamasisha  matumizi ya nishati safi ya kupikia na matumizi  salama na sahihi  ya umeme.

"Kwa  mkoa wa Shinyanga kuna vitongoji 2704 kati ya hivyo vitongoji 1180  ndiyo vinaumeme na vitongoji 1524 havina umeme lakini vitongoji 532 mkataba wake ulisainiwa mwezi Januari na wakandarasi wapo kwenye maeneo kwaajili ya kuanza utekelezaji hivi karibuni"amesema   Olutu.

Naibu  Waziri wa Nishati  Salome Makamba amesema   kufikia mwaka 2030 vitongoji  vyote vitakuwa na nishati ya umeme  na kuanza zoezi la kuunganishwa kwenye nyumba zao kwa gharama ya shilingi 27,000 kwa waishio maeneo ya vijijini ambapo matumaini wananchi wote wameelimika wananyumba za kisasa zinahitaji umeme.

Madiwani kutoka kata za Mwakata Ibrahimu Six na  Diwani wa kata ya  Kagongwa Ismail Masolwa   wamesema changamoto iliyopo nguzo  zinaletwa chache uhitaji ni mkubwa na maeneo mengine ya vitongoji ni umbali wa kilomita tisa hivyo wanaomba uunganishwaji wa haraka ufanyike kwenye vitongoji vyote.




Post a Comment

0 Comments