Wadau wa kiimo cha zao la pamba kutoka
katika wilaya ya Itilima na Bariadi wakiwa kwenye mdahalo wa kujadili
changamoto mbalimbali zinazolikabili zao la pamba mkoa wa Simiyu,ambapo
wamezitaka mamlaka zinazohusika na zao hilo kuacha kukaa tu ofisini
baadala yake waanze kuwatembelea wakulima vijijini ili kubaini
changamoto zilizopo likiwemo suala la bei,mbegu na madawa ya kuuwa
wadudu
waharibifu.
Wadau hao pia waliainisha changamoto mbalimbali ambazo zinachangia zao
hilo kuendelea kutokuwa na ubora hivyo kukosa thamani kuwa ni pamoja na
baadhi ya wakulima kuweka mchanga,sukari,chumvichumvi na maji ili
kuongeza uzito kufidia kilo zinazoibwa kwenye mizani ya pamba. wakati wa
kuuza kwa mawakala wa kampuni za kununua zao hilo.
|
0 Comments